WELCOME

Translate

Tuesday, March 15, 2016

UDICTETA HAUFAI KWA RAIYA WENU KUWENI VIONGOZI WAADILIFU

Nimetoka kuzungumza na 'reliable source' kutoka Wilaya ya Chake Chake, Mkoa wa Kusini Pemba, licha ya kuwa hakuna tamko rasmi la kuwataka kutokutoka nje baada ya ssa 2 usiku, lakini wanalazimika kubakia nyumbani mwao baada ya Sala ya Ishaa, hii inachagizwa na idadi kubwa ya polisi na wanajeshi waliotapakaa sehemu zote za kisiwa cha Pemba.
Nimemsikia Mohammed Aboud Mohammed, anasema wananchi wasiwe na hofu na idadi kubwa ya wanajeshi, akidai kuwa wapo katika mafunzo yao ya kawaida na hawahusiani na Uchaguzi isipokuwa tu mafunzo yao yameingiliana na kipindi cha uchaguzi.
Naweza kukubaliana na kauli ya Aboud (kama si ya kisiasa), lakini kama Serikali inayojali uhuru na haki za raia wake wanalazimika kutoa TAMKO lenye uzito unaostahiki, kuwahakikishia wananchi wake amani na utulivu na kuwataka waendelee na shughuli zao kama kawaida bila kuwawekea mipaka ya muda wakati hawajavunja sheria za nchi.
"Serikali inayowaogopa wananchi wake ni Serikali ya KIDIKTETA"!

No comments:

Post a Comment