WELCOME

Translate

Sunday, November 8, 2020

HATIMAE BARAZA LA WAWAKILISHI LAPATA SPIKA MPYA FUWATILIA BLOG YETU KWA HABARI ZAIDI

Wajumbe wa Baraza la wawakilishi jana wamemchagua Zuberi Ali Maulid kuwa Spika wa baraza la wawakilishi.
Zuberi ametetea tena nafasi yake ya uspika kwa kipindi chake cha pili kuliongoza baraza hilo.
Zuberi alipata kura 70 ambazo alipigiwa kura na wajumbe wote wa baraza hilo ambao walikua 70.
Spika huyo aliwabwaga wagombea wenzake wanne ambao wawili pia waligombea urais wa Zanzibar katika uchaguzi uliopita wa Octoba 28 mwaka huu.
Wagombeahao ni Hamad Mohd kutoka chama cha UPDP, katika uchaguzi wa uspika hakupata kura na Ameri Hassan Ameri kutoka chama cha Demokrasia makini ambae pia alikua mgombea Urais wa Zanzibar nae pia hakupata kura.
Wagombea wengine waliogombea nafasi ya Uspika ni Ali Makame kutoka chama cha CUF na Naima Salum Hamadi kutoka chama cha UDP ambao na wao hawakupata kura hata moja.

Saturday, May 16, 2020

JIPATIE PESA UKIWA NYUMBANI

Unacho takiwa kufanya nitakutumia link lafu utaifunguwa hiyo link utajisajili (REJISTETION) baada ya kumaliza usajili utabonyeza neno stat kuna box na chini zitakuja namba hizo namba unatakiwa uziweke kwenye hilo box hafu uta continyu kadri unvyo zidi kuweka namba ndivyo unavyo ongezewa pesa upande wa kushoto juu zitakuwepo pesa zako hafu unaweza kudroo pesa hizo kupitia acount uliyo nayo usisaha kuwaalika marafiki kupitia link hii 
https://aatmoney.xyz/549003688152879/

Sunday, March 15, 2020

M/MUNGU AMFANYIE WEPESI SHEE WETU HUSSEN NYUNDO

INNALILAHI WAINNAILAHI RAJIUN TUNASIKITILA KUTANGAZA KIFO CHA SHEIKH WETU HUSSEIN MARUFUU SHEIKH NYUNDO AMETANGULIA MBELE ZA KHALI MWENYEZIMUNGU AKULAZE MAHALI PEMA PEPONI AMIIN TULIKUPENDA LAKINI #ALLAH ALIKUPENDA ZAIDI MBELE YAKO NYUMA YETU ....R.I
P ...SHEIKH NYUNDO

Friday, February 14, 2020

KITUKO DUNIANI JAMAN

Afisa mmoja wa utalii nchini Afriika Kusini ambaye alifanikiwa kupata picha isio ya kawaida ya nyani akimbeba mwana wa simba katika mbuga ya kitaifa ya wanyamapori ya Kruger, amesema kwamba hajawaona tena wanyama hao tangu alipowapiga picha hiyo wiki iliopita.

Katika taarifa kwa BBC, mkurugenzi wa Kurt Safari , alisema kwamba msimu wa mvua umefanya kuwa vigumu kuwaona wanyama hao.

''Ni msimu wa mvua katika mbuga ya Kruger na miti imekuwa mikubwa huku nyasi zikiwa ndefu. Wakati nyani wanapoondoka katika barabara na kuingia katika nyasi , sio rahisi kuwaona''.

Sunday, February 9, 2020

BALAA YA MZIGE YAKARIBIA TZ

KILIMANJARO: NZIGE HUENDA WAKAINGIA TANZANIA
- Afisa Kilimo wa Wilaya ya Mwanga amesema wamepokea taarifa kuwa Nzige wapo Km 50 kufika ulipo mpaka wa Kenya na Tanzania
- Amewataka Wananchi kutoa taarifa mapema waonapo makundi ya Wadudu aina ya Panzi

Thursday, January 9, 2020

INALILAH AFRICA MASHARIKI YAONDOKEWA NA MWANAZUONI WAKE

AFRIKA MASHARIKI YAONDOKEWA NA MWANAZUONI SHEIKH HARITH SWAALEH AL MAAWY (1937 - 2020)
Kenya inaomboleza kifo cha msomi maarufu wa dini ya Kiislamu Sheikh Harith Swaleh aliyefariki siku ya Jumatano na kuzikwa siku ya Alhamisi mjini Mombasa Kenya.
Sheikh Harith Swaleh aliyezaliwa mwaka 1937, mjini Lamu ametoa mchango mkubwa kwa jamii ya Waislamu Afrika Mashariki na Afrika ya Kati
Ni mwana wa chuoni ambaye amesomesha wasomi wengi maarufu wa dini ya Kiislamu ambao wengi wao wamekuwa wanazuoni maarufu.
Kati yao ni Sheikh Ahmed Msallam,, Sheikh Sayyid Athman Saggaf,, Sheikh Muhammad Sharriff Famau miongoni mwa wengi wengineo.
Marehemu Aliandika vitabu vya dini maarufu Utangulizi wa Tafsiri ya QURAN, Hadithi za Mtume Muhammad S.A.W na vitabu vinginevyo.
Alipata mafunzo katika chuo cha kihistoria cha Riyadha mjini Lamu chuo ambacho kilikuwa miongoni mwa vyuo vya kwanza vya dini Afrika Mashariki

KESHO KUTAKUWA NA HALI YA KUPATWA MWEZI

TANZANIA KUSHUHUDIA KUPATWA KWA MWEZI KWA SAA NNE
Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini imetangaza kuwepo kwa tukio la kupatwa kwa mwezi litakaloonekana sehemu yote ya anga la Tanzania kesho Januari 10, kuanzia saa 2:07 usiku hadi saa 6:17 usiku.
Tukio hilo la kisayansi hutokea pale dunia inapopita katikati ya jua na mwezi na kusababisha kivuli katika uso wa mwezi.

MAMBO YANAZIDI KUPAMBA MOTO

Rais wa Marekani Donald Trump ameihakikishia nchi yake kuwa wakati wa utawala wake ataidhibiti Iran isiendelee na mpango wake wa nyuklia, akiitaja kuwa nchi inayofadhili ugaidi.

Akilihutubia taifa hilo jana, ikiwa ni siku moja tangu Iran ishambulie kambi mbili za jeshi la Marekani zilizoko nchini Iraq kama hatua ya kulipa kisasi cha kuuawa kwa kamanda wao, Qassem Soleimani, Trump amemuelezea kamanda huyo kama ‘gaidi hatari zaidi duniani’.

“Kama Mkuu wa Jeshi la Quds, Soleimani alihusika katika mashambulizi mengi, mikono yake ilikuwa imejaa damu za Wamarekani na Wairan na alitakiwa kuwa ameuawa siku nyingi zilizopita,” alisema Rais Trump.

“Kumuua Soleimani kumetuma ujumbe kwa magaidi wote duniani kuwa kama unathamini maisha yako mwenyewe hautatishia maisha ya watu wetu,” aliongeza.

Trump alisema kuwa Kamanda Soleimani alikuwa amepanga kufanya mashambulizi megine dhidi ya Wamarekani.

Katika hatua nyingine, Trump alisema kuwa mashambulizi ya kulipiza kisasi yaliyofanywa na majeshi la Iran kwenye kambi za kijeshi za Marekani hayakuwa na madhara yoyote.

Alidai hakuna mtu aliyefariki na hakukuwa na aliyepata majeraha makubwa. Kwa mujibu wa wake, Jeshi la Marekani lilipata taarifa mapema kuhusu kufanyika kwa mashambulizi hayo na likachukua tahadhari zote.

Lakini taarifa hiyo ya Rais Trump inakinzana na taarifa iliyotolewa na Iran, ambao wameeleza kuwa mashambulizi hayo yamesababisha vifo vya ‘magaidi 80 wa Marekani’.

Iran imeapa kuendelea kulipa kisasi dhidi ya hatua za Marekani. Kifo cha Kamanda Soleimani ambaye anaheshima kubwa nchini Iran kama mwanamapinduzi na shujaa kimeamsha hasira za nchi hiyo, akizikwa na maelfu.

Iran, imetangaza rasmi kuvunja mkataba wa mpango wa nyuklia kati yake ya Marekani, na inaendelea na uzalishaji kama kawaida.

Rais Trump alidai kuwa ili kuidhibiti Iran isiendelee na mpango wake wa Nyuklia, wataweka vikwazo vipya vya kiuchumi dhidi ya nchi hiyo; na kwamba Marekani inaweza kuishi bila kutegemea mafuta kutoka Mashariki ya Kati.

SHIDA KWA MMAREKANI

'DRONE', NDEGE HATARI ISIYOKUWA NA RUBANI
1. UTANGULIZI
KATIKA andiko hili ambalo mdau una nafasi huru kuchangia mawazo yako, tutaona jinsi ndege ya kijeshi isiyokuwa na rubani, yaani 'Drone,' inavyofanyakazi, hususan katika kubaini mlengwa na kumshambulia kwa makombora.
Pia, tutaona baadhi ya madhara makubwa ambayo yamekuwa yakisababishwa na mashambulizi ya ndege hizo pale zinaposhambulia kile kinachoitwa magaidi.
2. MAANA YA 'DRONE'
Jina drone ni la lugha ya Kiingereza likimaanisha nyuki-dume, ambao jukumu lao ni kuwapanda malkia wa nyuki kwa lengo la kupandikiza mbegu zao.
Kwa kutumia nguvu kubwa nyuki-dume hao hupandikiza hizo mbegu zao kwa malkia kwa mara moja tu, ambapo muda mfupi baadaye madume hao hufa.
Hiyo ikiwa na maana kwamba, nyuki hao dume hupoteza maisha baada ya kupenyeza mbegu zao kwa malkia wa nyuki.
Hivyo, kutokana na hali hiyo ya 'drone-nyuki,' ndio maana katika siku za nyuma 'drone-ndege' zilikuwa zikipoteza uwezo wa kwendelea kutumika baada ya kushambulia adui mara moja; sawa na 'drone-nyuki.'
3. AINA ZA DRONE-NDEGE
Drone ndege zipo za aina nyingi, zikiwemo kubwa za kubeba mizigo mizito ya kijeshi, za kuzima moto, za kutafiti mazingira ya hali ya hewa, nk.
Aidha, hapa tutaangalia drone ndogo ambazo ni za matumizi ya kijeshi, hususan katika kushambulia maadui wanaolengwa.
Uzito wa hizo Drone ndogo za kivita ni kilo takribani 700, sawa na uzito wa basi dogo la abiria, yaani Hiace, ambapo drone ikiwa na makombora uzito huwa huongezeka kuwa kilo takribani 1000.
Kadhalika, gharama ya kununua Drone moja ya kijeshi ni kati ya dola za Marekani milioni 4 (sh. bilioni 9.2), ambapo Drone kubwa huweza kugharamu hadi dola milioni 120 (sh. bilioni 276).
Drone hutumika pale ambapo mazingira hayaruhusu binadamu kutumika kumshambulia adui, ambapo mpaka wakati huu serikali ya Marekani ndiyo inaongoza katika kutumia ndege hizo kushambulia na kuua.
Mathalani, idhini ya kutumia drone kushambulia popote duniani hutolewa na Rais wa nchi hiyo, wakati huu ni Donald Trump, huku pia mitambo ya kuziongoza ndege hizo ikiwa ndani kabisa ya nchi hiyo ya Marekani.
4. KITUO KIKUU CHA DRONE
Mojawapo ya mambo ambayo yatakushangaza msomaji ni kuwa kituo kikuu cha kuongoza ndege hizo za drobe za Marekani kipo katika Jimbo la Nevada la nchini humo.
Kituo kingine maarufu kipo katika mji wa Kandahar, nchini Afghanistan.
Mitambo ya kuongoza ndege hizo ina uwezo wa kuona kila kona ya dunia, huku ndege hizo zikiwa zimesambazwa katika vituo mbalimbali vya kijeshi vya Marekani vilivyotapakaa katika nchi mbalimbali, ikiwemo Barani Afrika.
Mathalani, katika chumba kimojawapo utakuta kuna vijana watalaamu ambao hutumia kompyuta kufuatilia nyendo mbalimbali za walengwa wa mashambulizi kutoka kwa drone.
Kimsingi, kinachofanyika ni makachero wa Marekani katika maeneo mbalimbali husika kufuatilia kwa makini nyendo za walengwa, hadi kufahamu wapi walipo katika wakati muafaka.
Kachero au makachero husika hutumia simu maalumu kutoa taarifa katika kituo kilichopo jirani na kituo kikuu chenye drone, ambapo kituo hicho hutuma haraka taarifa kamili kwa magwiji wa kompyuta za kuongoza drone kule Nevada.
Magwiji hao kwa kutumia mitambo ya setelaiti zilizopo angani huweza kutafuta na kuona eneo tajwa husika, ikiwemo mlengwa au walengwa, jengo au gari lililombeba mlengwa au walengwa.
Mara moja mitambo ya drone hujazwa taarifa hizo, yaani 'data' husika na kuamriwa kuanza safari kwelekea kwenye eneo alipo mlengwa au walengwa.
Wastani wa kasi ya drone kwenda eneo husika ni kati ya kilomita 250 na 350 kwa saa, na hivyo kuwa na uweza wa kuwasili katika shabaha husika ndani ya muda mfupi.
Kadhalika, ndege hiyo ina uwezo wa kusafiri umbali mrefu wa kilomita 2500 kumfuata adui, huku pia ikiwa na uwezo wa kumshambulia ikiwa umbali wa kilomita 8 kutoka angani hadi ardhini.
Pia, Drone ina uwezo wa kukaa angani kwa muda mrefu hadi kwa saa takribani 12, ikiranda randa angani kumtafuta adui au kuchunguza nyendo za washukiwa wa uhalifu, hususan ugaidi.
Waongozaji kule Nevada au Kandahar huweza kuiona ndege hiyo na pia kuona shabaha inayolengwa, ambapo huwa rahisi kuelekeza drone kulishukia eneo husika na kufyatua kombora dhidi ya shabaha inayolengwa.
Aidha, kwa mjibu wa mtaalamu wa kuongoza drone nchini Marekani ambaye sasa ni mstaafu, hukariri na gazeti la Guardian la nchini Uingereza akisema kuwa lugha inayotumika kati ya wao waogozaji (waliopo Nevada) na warushaji wa drone (mfano waliopo Syria au Afghanistan au Irak, nk) ni lugha ya kificho.
Mathalani, kachero huyo hukaririwa akisema kwamba waongozaji wa Drone wakishaona shabaha inayowindwa huweza kuwaambia warushaji wa ndege hiyo kuwa "nyasi zimechipua tayari kuvunwa," ikimaanishwa kuwa anayewindwa ameonekana mahali alipo.
Mara moja warushaji wa drone huwaambia waongozaji kuwa "kama gugu limeota, tuwahi kulikata," ikimaanishwa kuwa ni wakati muafaka kutuma Drone kushambulia.
Mara moja warushaji wanaporusha ndege hiyo kwenda angani, waongozaji "hudaka" masafa yake kwa njia ya setelaiti na kuanza kuidhibiti drone husika hadi kwenye eneo la shabaha husika.
Drone hubaki kuranda randa katika eneo hilo hadi pale shabaha husika inapoonekana wazi, ambapo ndege hiyo huishukia na kufyatua kombora.
5. WATOTO NI KINGA DHIDI YA SHAMBULIO LA DRONE
Mara kadhaa baadhi ya washukiwa wa ugaidi wamewahi kuwatumia watoto wao kama kinga, wakitambua kuwa kanuni za kimataifa zinakataza kuuwa watoto vitani.
Hivyo, mshukiwa wa ugaidi anapoonekana akiandamana na mtoto shambulio la drone huahirishwa.
Hiyo ni kwa sababu ya kuepusha lawama kwa serikali yenye kutumia ndege hizo dhidi ya watuhumiwa wa ugaidi, au washukiwa wowote ambao hutakiwa kushambuliwa.
6. NCHI ZENYE DRONE
Mpaka sasa ni nchi chache tu zenye kutumia kwa wingi ndege hizo zisizokuwa na rubani, ikiwemo Marekani, Israel, China, Iran, Italia, India, Pakistan, Urusi, Uturuki, Poland, na Iran.
Baadhi ya nchi hizo huunda zenyewe ndege hizo na nchi zingine ununua ambapo mwaka jana 2019, matumizi ya ndege hizo yaliongezeka mno.
Nchi ambazo mashambulizi ya ndege hizo ni mengi ni pamoja na Afghanistan, Pakistan, Syria, Irak, Somalia, and Yemen, ambapo pia idadi ya mashambulizi inazidi kuongezeka kila siku.
7. MADHARA YA DRONE
Kuanzia mwaka 2015 hadi 2019, idadi ya mashambulizi kutoka kwenye Drone za Marekani nchini Pakistan dhidi ya kile kinachodaiwa kuwa ni kuangamiza magaidi, yaliua watu 3,949.
Kwa mujibu wa taasisi za Marekani zinazopinga nchi hiyo kutumia ndege hizo kuua watu, jumla ya raia waliopoteza maisha nchini Pakistan ni 962.
Raia hao walipoteza maisha wakati ndege hizo zikishambulia wale waliodaiwa kuwa ni magaidi, au raia hao kudhaniwa kuwa magaidi dhidi ya maslahi ya Marekani.
Nchini Yemen ambapo kuna vita ya wenyewe kwa wenyewe, huku serikali ya Marekani ikiunga mkono upande mmoja, jumla ya mashambulizi kutoka ndege hizo yalikuwa 206, ambapo jumla ya watu waliouawa ni 1,1174, wakiwemo raia 158.
Aidha, nchini Somalia ambapo Marekani inawakabili wanamgambo wa Al-Shabaab dhidi ya serikali ya nchini humo, jumla ya mashambulizi yalikuwa 23, ambapo jumla ya vifo ilikuwa 116, wakiwemo raia 12.
8. MASHAMBULIZI YA DRONE DHIDI YA "MAGAIDI"
Katika kuhitimisha ngoja tuangalie baadhi ya wahanga wakuu wa mashambulizi hayo ya Drone, walivyopoteza maisha kutokana na kuvamiwa na ndege hizo za Drone:-
i). Anwar al-Awlak (40)
Huyu alikuwa mwalimu wa mafundisho ya kiimani katika eneo la Mashariki ya Kati na barani Asia.
Serikali ya Marekani ilimtuhumu kwa kuajiri wanamgambo wapya wa kikundi cha kigaidi cha Al-qaed nchini Yemen, ambapo drone zilianza kumsaka.
Baada ya kumtafuta kwa muda mrefu, huku mara kadhaa shambulizi dhidi yake likiahirishwa kwa vile alikuwa anamtumia mtoto wake (mwenye umri wa miaka 16 raia wa Marekani) kama kinga, siku moja alionekana akipata chakula katika mgahawa mmoja nchini Yemen.
Drone ilitumwa na kuwasili katika eneo hilo na pia kuonekana angani, mwalimu huyo na wenzake walikimbilia kwenye gari lao na kuanza kutoroka wakiwa ndani ya gari hilo katika barabara kuu.
Hilo likawa ni kosa la kiufundi, kwani drone iliwaona na kulifuata gani hilo na kulishambulia kwa kombora kutoka umbali wa kilomita 7 angani.
Watu wote ndani ya gari hilo walipoteza maisha, akiwemo mwalimu Anwar, na mwandishi wa habari aliyedaiwa kuwa mwajiriwa wa kikundi Al-qaed.
ii). Mohammed Emwazi a.k.a Muhammad Jassim Abdulkarim Olayan al-Dhafiri a.k.a Jihad John (27)
Huyu ni yule ambaye kupitia video kadhaa miaka 2014 na 2015 alikuwa akionekana akiwakata vichwa raia wa Marekani waishio Mashariki ya Kati kabla ya kifo chake.
Miongoni mwa matukio aliyohusika ni mauaji nchini Syria ya raia 6 wa Mataifa ya Magharibi na 2 wa nchini Japan, wakiwemo waandishi wa habari na watoa misaada kwa wahanga wa vita.
Akiwa mwarabu mwenye uraia wa nchini Uingereza, John alitokea kuwa muuaji maarufu Mashariki ya Kati, ambapo alikuwa na mtindo wa kuwakata vìchwa watu hao huku matukio hayo yakioneshwa kwenye video.
Aidha, kutokana na vitendo hivyo vya kikatili, vilisababisha "Jihad John" kusakwa kwa upana zaidi, huku drone 3 zikitumika katika operesheni ya kumtafuta.
Siku yake iliwadia wakati akiwa anatoka kwenye jengo moja nchini Syria ili aingie kwenye gari lake, ambapo hizo drone 3 zilimuona na kumshukia kwa makombora 3 kwa pamoja na kumsambaratisha sawia.
iii). Abu Hussain al-Britani (21),
Huyu alikuwa ni mzaliwa wa nchini Uingereza mwenye asili ya nchini Pakistan, akiwa ni mwana propaganda na mtaalamu wa kompyuta za kikundi cha Al-qaeda.
Siku ya kwanza kushambuliwa nchini Irak drone ilimkosa, lakini kombara kutoka ndege hiyo liliua raia 3 na kujeruhi 5, huku yeye akisalimika na kutoroka kutoka eneo hilo.
Siku 10 baadaye ilitumika mbinu tofauti ili kumpata, ambayo ni kuunganisha mawasiliano ya simu yake na masafa ya setelaiti yanayoongoza drone.
Alipopigiwa simu tu, drone ilinasa mawimbi ya sauti kutoka kwenye simu yake na kuyafuata hadi ilipomuona kwenye kituo cha petroli akijaza mafuta kwenye gari lake.
Kombora kutoka kwenye drone hiyo lilisababisha kifo chake, pamoja wa watu kadhaa, wakiwemo 3 waliodaiwa kuwa walinzi wake.
iv). Kamal Derwish (29),
Huyu alikuwa raia wa Marekani mwenye asili ya nchini Yemen, ambaye alituhumiwa kuhusika katika kutoa mafunzo kwa magaidi nyumbani kwake nchini Marekani, kabla ya kutorokea Yemen.
Ikijibu shutuma za Wamarekani kuwa drone ya nchi hiyo imeua raia wao nchini Yemen, serikali ya Marekani ilidai kuwa Derwish alikuwa tishio kwa maslahi ya taifa hilo katika eneo la Mashariki ya Kati.
Siku ya tukio la kuuawa, mwanaharakati huyo alikuwa anasafiri na wenzake 4 kwenye gari lao kuitikia wito wa kwenda kukutana na wanaharakati wenzake katika eneo mojawapo la jangwa la nchini Yemen.
Baada ya kufika katika eneo husika, dereva wa gari lao alipiga simu kwa wenzao kuwa tayari wamefika katika sehemu ya kukutania.
Bila kutambua kuwa huo ulikuwa ni mtego, badala yake drone ilinasa masafa ya simu hiyo na kuyafuata hadi kutokea walipokuwa watu hao.
Drone hiyo ilifyatua kombora ambalo lilisambaratisha gari hilo, na kuua watu wote 5, akiwemo Derwish na dereva wao.
Hakika, matukio ya aina hiyo ni mengi mno, ambapo kwa mujibu wa utafiti wa televisheni ya Fox News nchini Marekani, asilimia 63 ya wananchi wa nchi hiyo wanapinga matumizi ya Drone, asilimia 32 wanakubali, na asilimia 5 hawana majibu

Wednesday, January 8, 2020

TRAMP ASEMA

Rais wa Marekani, Donald Trump amesisitiza kuwa hakuna mwanajeshi wa Marekani aliyekufa kwenye shambulizi la makombora lililofanywa kwenye kambi mbili za jeshi hilo zilizopo nchini Iraq 

MAREKANI YASHINDWA KUZUIYA KOMBORA DHIDI YA IRAN

Vikosi vya Marekani vimeshindwa kuzuia kombora lolote la jeshi la IRGC la Iran lililorushwa dhidi ya kambi za Marekani nchini Iraq. Naibu mkuu wa operesheni wa jeshi hilo Brigedi Jenerali Abbas Nilforoushan amesema makombora ya Iran yamelenga kambi hizo kwa usahihi. Pia amesema majeshi ya Marekani japokuwa yamejiandaa vizuri kabla ya mashambulizi ya Iran, lakini wameshindwa kabisa kuzuia kombora lolote.

MASHIRIKA YA NDEGE YASITISHA KUPITA KATIKA ANGA YA IRAN NA IRAQ

Mashirika mbalimbali ya ndege duniani yamekwepa anga za Iran na Iraq kufuatia mzozo wa Marekani na Iran.
Kufuatia shambulio la kombora la Iran dhidi ya kambi za kijeshi ambapo vikosi vya jeshi la Marekani na vikosi vya muungano viliweka kambi, mashirika kadhaa ya ndege yamebadili njia zao kutoka anga la Iran na Iraq.
Mara baada ya shambulio hilo, Mamlaka za usafirishaji wa anga nchini Marekani zilitangaza kuzuia mashirika yake kupita katika anga za Iraq, Iran, Ghuba ya Oman na bahari kati ya Iran na Saudi Arabia.
Kando na Marekani, mashirika kadhaa ya ndege ya Asia na Ulaya pia yameeleza kuepuka anga la Iran.
Wakala wa habari nchini India, Asian News International (ANI), lilinukuu vyanzo vya serikali kwamba mashirika yote ya ndege ya India yametakiwa kuepuka anga za Iran, Iraqi na Ghuba kufuatia mvutano katika eneo hilo.
Shirika la ndege la Singapore (Singapore Airlines) pia limebadili njia zake kukwepa anga la Iran.
"Kwa kuzingatia yanayoendelea kati ya Amerika na Iran, ndege zote za Singapore Airlines ndani na nje ya Ulaya zinaelekezwa kuepuka anga la Iran," shirika hilo lilisema.
"Tunafuatilia hali hiyo kwa karibu na tutafanya marekebisho sahihi kwa njia zetu ikiwa ni lazima," liliongeza.
Shirika kubwa zaidi la usafiri wa anga nchini Taiwan, China Airlines ilisema katika taarifa kwamba itaendelea kuangalia hali inavyokwenda na kisha kurekebisha njia ipasavyo, liliripoti Reuters.
Shirika lingine la Taiwan, EVA Air, na Malaysia Airlines pia yamesema wanaepuka kuruka juu ya anga la Iran.
Shirika la Korean Air limesema lilikuwa likiepuka anga la Iran na Iraq kabla ya shambulio dhidi ya kambi za Marekani.
Shirika la Australia, Qantas, limesema lilibadilisha njia yake ya London kwenda Perth, Australia, kuepuka anga za Iran na Iraq hadi taarifa zaidi zitakapotolewa, limeripoti Associated Press.
Wakala wa anga wa Urusi, Rosaviatsia, pia limetoa pendekezo rasmi kwa mashirika yote ya ndege ya Urusi kujiepusha kuruka juu ya Iran, Iraqi, Ghuba ya Uajemi na Ghuba ya Oman "kutokana na hatari zilizopo kwa usalama wa ndege za kimataifa."
Shirika la ndege la Ujerumani, Lufthansa, limefuta safari yake kutoka Frankfurt kwenda Tehran Jumatano kwa kuzingatia hali ya sasa, limeripoti Associated Press.
Shirika la ndege la Ufaransa Air France lilisema kampuni hiyo imesimamisha safari zake juu ya anga la Iraq na Iran, limeripoti Reuters.
"Mipango ya ndege itarekebishwa kwa wakati kulingana na maamuzi ya viongozi wa Ufaransa na wa kikanda, ili kuhakikisha kiwango cha juu cha usalama wa ndege", Air France ilisema katika taarifa yake
Shirika linalomilikiwa na Falme za Kiarabu (UAE), Flydubai, limefuta safari iliyopangwa Jumatano kutoka Dubai kwenda Baghdad, lakini likiendelea safari kwenda Basra na Najaf.
Safari za shirika la Emirates kati ya Dubai na Baghdad zimefutwa.
Shirika la Qatar Airways, hata hivyo, lilisema ndege zake kwenda Iraq zilikuwa zinafanya kazi kawaida.

MAREKANI

Wanajeshi wa warekani wakiwa wanaagana na familia zao na kuelekea nchini iraq 

KIMENUKA SASA

Rais wa Iran, Hassan Rohani anatarajia kulihutubia taifa Jumatano wiki hii, hotuba ambayo itarushwa hewani moja kwa moja kwenye televisheni ya serikali, kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters.

Hotuba hiyo inakuja saa chache baada ya jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu kurusha makombora kadhaa dhidi ya kambi mbili za jeshi zinazotumiwa na Marekani nchini Iraq.

Pentagon inasema kuwa karibu kambi mbili zilishambuliwa, mjini Irbil na Al Asad.

Tayari baadhi ya wananchi wa Iraq wamebaini kwamba mashambulizi hayo ya iran nchini Iraq yanavunja uhuru wa nchi yao.

Runinga ya kitaifa ya Iran imetangaza kuwa shambulio hilo ni la kulipiza kisasi mauaji ya kamanda mkuu Qasem Soleimani aliyeuawa katika shambulio la ndege isiyokuwa na rubani mjini Baghdad, kufuatia agizo la rais wa Marekani Donald Trump.

Kuuwawa kwa Soleimani Januari 3 kulizorotesha uhusiano kati ya Iran na Marekani.

Jenerali Soleimani - alikuwa kiongozi wa oparesheni ya kijeshi ya Iran katika eneo la mashariki ya kati - lakini serikali ya Marekani ilimuona kuwa gaidi, ambaye alihusika na vifo vya mamia ya wanajeshi wake na kwamba alikuwa akipanga shambulio "hatari".

Tuesday, October 1, 2019

NIMERUDI TENA

Baada ya takribani miaka 2 nikuwa sipo ila nashukuru mungu tutakuwa p1

Tuesday, March 15, 2016

UDICTETA HAUFAI KWA RAIYA WENU KUWENI VIONGOZI WAADILIFU

Nimetoka kuzungumza na 'reliable source' kutoka Wilaya ya Chake Chake, Mkoa wa Kusini Pemba, licha ya kuwa hakuna tamko rasmi la kuwataka kutokutoka nje baada ya ssa 2 usiku, lakini wanalazimika kubakia nyumbani mwao baada ya Sala ya Ishaa, hii inachagizwa na idadi kubwa ya polisi na wanajeshi waliotapakaa sehemu zote za kisiwa cha Pemba.
Nimemsikia Mohammed Aboud Mohammed, anasema wananchi wasiwe na hofu na idadi kubwa ya wanajeshi, akidai kuwa wapo katika mafunzo yao ya kawaida na hawahusiani na Uchaguzi isipokuwa tu mafunzo yao yameingiliana na kipindi cha uchaguzi.
Naweza kukubaliana na kauli ya Aboud (kama si ya kisiasa), lakini kama Serikali inayojali uhuru na haki za raia wake wanalazimika kutoa TAMKO lenye uzito unaostahiki, kuwahakikishia wananchi wake amani na utulivu na kuwataka waendelee na shughuli zao kama kawaida bila kuwawekea mipaka ya muda wakati hawajavunja sheria za nchi.
"Serikali inayowaogopa wananchi wake ni Serikali ya KIDIKTETA"!


Wednesday, October 28, 2015

KIMENUKA TENA ZANZIBAR

KWA HALI ISIYO YA KAWAIDA NA MARA YA KWANZA VISIWANI ZANZIBAR  UCHAGUZI WA HUO UMEHAIRISHWA MUDA MFUPI BAADA YA KUSHINDWA KUTANGAZA KATIKA KINYANGANYIRO CHA UGOMBEA URAISI ULIO FANYIKA VISIWAVI HUMU  HATUJUWI NI KWASABABU GANI ILIO PELEKEA KUHAIRISHWA  AU NI KWASABABU YA KUSHINWA KWA CHAMA TAWALA VISIWANI HUMU ILA WANACHO KITAFUTA HAPA WAHAFIDHINA WA ZANZIBAR NI KUREJESHA MAUMIVU YA WANZANZIBAR  NA KUIMWAGA TENA DAMU YA WANZANZIBAR ILA KWA MPANGO HUU NIBORA WATU WAFE WOTE KULIKO KUWACHEZEA TENA WANZANZIBAR TUNATOWA TAMKO KWA VIONGOZI WETU WA NCHI HII MWAKA HUU HAMTAKUWA  NA PAKUKIMBILIA MJUWE IKIMWAGIKA ZAMU YA WAZANZIBAR BASI NA NYINYI VIONGOZI WOTE MTAFUTE NCHI YA KUKIMBILIA TUMECHOKA KUTUNYANYASA KUTUUWA NA TUNATOWA TAMKO KWA VIKOSI VYA SMZ HAMJAAJIRIWA KWA KUWAUWA WAZANZIBAR NYINYI NYOTE TUNAKUJUWENI MNAISHI MITAANI KWETU ILA KAMA MNATAKA DAMU IMWAGIKE ENDELEENI KUWAPIGA WAZANZIBARI NA WAPEMBA TUSIJE KULAUMIANA MBELE YA SAFARI YANGU NI HAYO TU

Friday, July 24, 2015

A HUNDRED YEARS FROM NOW

“A hundred years from now when you are alone in your grave, no one will care how much money you had,what car you drove or what kind of house you lived in.The only thing that will matter then will be your righteous deeds."Abdulbary Yahya.
Yaa Allah give us strength to do righteous deeds,amen.

Wednesday, July 22, 2015

CHUO KIMOJA KIKUU NCHINI UWENGEREZA KIMESEMA KUWA UTAFITI WALIO UFANYA NYARAKA ZA ZAMANI KATIKA MAKTABA YAKE IMEONWSHA KUWA HUWENDA ZIKAWA ZA ZAMANI SANA

Chuo kimoja kikuu nchini Uingereza kimesema kuwa utafiti waliofanyia nyaraka za zamani katika maktaba yake, umeonesha kuwa huenda zikawa nakala za zamani sana duniani za koran. Watafiti katika chuo cha Birmingham wanasma kuwa walishangazwa sana walipogundua kupitia uchunguzi wa miale ya radiocarbon kuwa nyaraka hizo kutoka kitabu kitakatifu cha waislamu Koran, zina umri wa zaidi ya miaka 1300,
wanasema kuwa mwandishi wa nyaraka hizo huenda alikutana ana kwa ana na mtume Muhammadau alikuwa miongoni mwa wanafunzi wake.
Nyaraka hizo ni miongoni mwa maelfu zingine za kale kutoka mashariki ya kati ambazo zilimilikiwa na mwana historia mzawa wa Iraq, Alphonse Mingana, aliyekabidhi kwa chuo kikuu hicho cha Birmingham katika miaka ya ishirini.

AWALI IDARA YA POLICE NCHINI KENYA ILIKUWA WAMETANGAZA KUWA ANGA YOTE YA KENYA ITAFUNGWA

Awali idara ya polisi nchini Kenya ilikuwa imetangaza kuwa anga yote ya Kenya itafungwa kwa muda wa siku tatu kabla ya ziara hiyo lakini kwa mujibu wa shirika la KCAA ndege zote zinazopaa chini ya futi elfu ishirini hazitaruhusiwa kutua katika uwanja wa Jomo Kenyatta na uwanja wa wilson mjini Nairobi kuanzia siku ya Ijumaa hadi siku ya jumatatu, wakati wa kongamano la kimataifa ya ujasiriamali litakalofanyika mjini Nairobi.
Agizo hilo sasa linamaanisha ndege zote ndogo ndogo ambazo uhudumu kati ya Nairobi na Somalia na viwanja vingine vidogo vidogo katika kanda ya Afrika Mashariki, havitaruhusiwa kutua Nairobi hadi mkutano huo utakapomalizika.
Rais wa Marekani Barrack Obama anatarajiwa mjini Nairobi siku ya Ijumaa usiku ambapo anatarajiwa kuwa mwenyeji wa kongamano hilo la kibiashara kwa pamoja na mwenyeji wake rais uhuru Kenyatta.

SHIRIKA LA NDEGE LA KENYA LIMESEMA LITASITISHA SAFARI YAKE ZOTE ILI KUPISHA ZIARA YA RAISI OBAMA

Shirika linalosimamia safari za ndege nchini Kenya, KCAA, limetangaza kuwa anga ya Kenya itafungwa kwa muda wa dakika hamsini siku ya Ijumaa wiki hii ili kuruhusu ndege ya rais wa Marekani Barrack Obama kutua katika uwanja wa kimataifa wa ndege wa Jomo Kenyatta mjini Nairobi.
Kwa mujibu wa shirika hilo, agizo hilo litatekelezwa katika viwanja vyote vya ndege nchini Kenya na kuwa anga hiyo itafunguliwa muda tu pale ndege hiyo ya rais Obama itakapokuwa imetua.
Shirika hilo limesema kuwa limeyaandikia mashirika yote ya ndege na pia kampuni zote za usafiri kuhusiana na agizo hilo na kuwa safari za ndege kadhaa zitacheleweshwa siku hiyo na pia siku ya jumapili wakati rais Obama atakapokuwa akiondoka nchini Kenya kuelekea Ethiopia kwa muda wa dakika arubaini.

LEO NDIO LEO MGOMBEA WA URAIS KUPITIA UKAWA LEO NDIO ANATANGWAZWA

Msemaji wa CHADEMA, Tumaini Makene amesema mkutano mkubwa utakaofanyika Mwanza leo ndiyo utakaotegua nani atakayepeperusha bendera ya UKAWA katika nafasi ya Urais

Monday, July 20, 2015

RAIS J.KIKWETE AKIWEKA SAIN YA JARIDA LA MPANGO



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini kwenye jarida la Mpango wa Modenaizesheni ya Sekta ya Mifugo baada ya kuuzindua mpango huo leo Jumatatu Julai 20, 2015

WAZIRI WA SAYANCE AKISALIMIANA NA WACHEZAJI WA WAWI BOYS


WAZIRI wa Mawasiliano, Sayansi na Teknlojia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Pro: Makame Mnyaa Mbarawa, akisalimiana na wachezaji wa timu ya Wawi star, kabla ya kuanza kwa mchezo wa fainali ya kuwania kombe la CCM jimbo la Wawi, dhidi ya Fidel castro, uliochezwa uwanja wa Gombani Chake chake Pemba, ambapo Fidel ilitazwa ubingwa (Picha na Haji Nassor, Pe

KUKOSEKANA MCHEZAJI SALUM ABDALLA KWENYE KOMBE LA CCM KATIKA JIMBO LA WAWI

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh1b9lUgAEsrLmQL9GfuuWtndQVbk2R0zaG5UInWHRVRrI3LJPOkWNc6kQwGX9RRzEyzxwgQv2gROCGGIbpgLyHv_U3oM8F-V_kRhyphenhyphen9glwrjVAchntRWccJDUNHnQ8QT_DpXb9_JCf7vuQ/s640/DSC_9436.JPG  
KUKOSEKANA kwa machela maalumu kwenye michuano mbali mbali inayochezwa uwanja wa Gombani, husababisha kwa wachezaji kubebana wenyewe, kama juzi kwenye michuano ya kuwania kombe la CCM jimbo la Wawi, ambapo timu ya Wawi star ikimtoa mchezaji wao Salum Abdalla baada ya kupata majeraha, (Picha na Haji Nassor, Pemba).


MH MAKAME MNYAA AKISALIMIANA NA WAZAFUNZI WA FIDEL CASTRO PEMBA

 
WAZIRI wa Mawasiliano, Sayansi na Teknlojia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Pro: Makame Mnyaa Mbarawa, akisalimiana na wachezaji wa timu ya Fidel Castro, kabla ya kuanza kwa mchezo wa fainali ya kuwania kombe la CCM jimbo la Wawi, dhidi ya Wawi star, uliochezwa uwanja wa Gombani Chake chake Pemba, ambapo Fidel iliibuka na ubingwa, (Picha na Haji Nassor, Pemba).


MKURUGENZI WA ZAWA ZANZIBAR NA MH BALOZI SEIF ALL IDD





 Mkurugenzi Uzalishaji Maji wa Mamlaka ya Maji Zanzibar {ZAWA } Mhandisi Moh’d Elyas aliyenyanyua mkono akimpatia maelezo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif kazi zilizobakia katika kukamilisha Miundombinu ya ujenzi wa kisima cha Maji safi katika Kijiji cha Kinduni Wilaya ya Kaskazini “B”.

KIONGOZI MAHIRI

in my life I never could get mad as a competent leader Yussuf masauni is a leader who does not discriminate in its color inspiration tribe nor religion and are responsive in the community and is implementing in infrastructure in the education and empowerment of youth

mohammed suleiman akikabidhi fedha za kuchukulia fomu ya ubunge


Mgombea Jimbo la Malindi Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi Ndg Mohammed Suleiman Omar akikabidhi fedha kwa ajili ya malipo ya fomu ya Ubunge wa Jimbo la Malindi Zanzibar kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Mjini Ndg Abdurahaman Kasongo.

Mohammed suleiman ajitosa kugombea ubunge jimbo la malindi zanzibar

Mohammed Suleiman Omar Ajitosa Kugombea Ubunge Jimbo la Malindi Zanzibar

  

 Katibu wa CCM Wilaya ya Mjini Ndg Abdurahamani Kasongo, akipitia Kadi ya Mwananchama wa CCM Ndg Mohammed Suleiman aliyejitokeza kugombea Ubunge Jimbo la Malindi Zanzibar. 



MBUNGE WA MUHABWE MHE MKOSAMALI ANASEMA WANAMUWINDA YEYE ATABAKI KUWA UKAWA

Mbunge wa Muhambwe, Mhe Felix Mkosamali amesema wanamuwinda sana lakini hawawezi kumpata, atabaki UKAWA kwasababu hawezi kujiunga na vyama vidogo vidogo ili kuisaidia CCM kupita kiurahisi.
Nini ungependa kumwambia mbunge huyu?
https://fbcdn-sphotos-h-a.akamaihd.net/hphotos-ak-xtp1/v/t1.0-9/p480x480/11755210_1271969386150810_7442406566304705062_n.jpg?oh=b403888a9109b8426da611520b781e5b&oe=5656EF70&__gda__=1443858005_87a46158c0f8d83cbca3270ebe4ebe94